Burudani

Baada ya G Nako kufanya cover ya Seduce Me, ‘mambo ya team yakae mbali’

Msanii wa kundi la Weusi, G Nako ameelezea mafanikio ya cover ya ngoma Seduce Me ya Alikiba aliyofanya.

G Nako ambaye kwa sasa anatamba na ngoma ‘Energy’ amekiambia kipindi cha Clouds E kuwa mapokezi ya ngoma hiyo yamekuwa makubwa lakini mambo ya u-team katika muziki hayataki.

“Kwanza kabisa sitaki masuala ya ma-team, kuna vitu kidogo yanakuwa yanatuwekea mipaka, mambo ya team yakae mbali halafu muziki mzuri ndio uongee lakini so far mapokezi ni makubwa” amesema G Nako.

G Nako anaungana na producer Man Water na wasanii wengine mbali mbali ambao wamefanya cover ya ngoma hiyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents