Burudani
Beyonce ndiye staa aliyetafutwa zaidi kwenye Google
Beyonce ndiye msanii wa kike aliyetafutwa zaidi kwenye Google mwaka huu kwa upande wa Uingereza.
Muimbaji huyo amekuwa kwenye spotlight katika kipindi cha miezi 12 iliyopita kutokana na tetesi za kuyumba kwa ndoa yake na Jay Z. Kingine ni baada ya mrembo huyo kutoa album ya surprise na ziara yake na mumewe ya ‘On The Run’
Hii ni orodha nzima:
Mastaa wa kike waliotafutwa zaidi kwenye Google:
1) Beyonce
2) Jennifer Lawrence
3) Katy Perry
4) Ariana Grande
5) Taylor Swift
Mastaa wa kiume waliotafutwa zaidi kwenye Google:
1) Ed Sheeran
2) Jay Z
3) Harry Styles
4) Benedict Cumberbatch
5) David Beckham