Habari
Bonta: Utazomewa ukisema mimi sio conscious, avunja ukimya kwa ngoma mpya ‘Mtaani watu Buuu’ (Audio)
Rapper wa kampuni ya Weusi, Bonta, amevunja ukimya kwa kuachia wimbo mpya, ‘Mtaani watu Buuu’. Katika wimbo huo aliomshirikisha G-Nako na kutayarishwa na producer Mona Gangster, rapper huyo anajaribu kuwakumbusha kuwa watu bado ni conscious rapper na kama ukibisha watu watakuzomea.
Bonta akiwa na Adili
“Unaposema mimi sio conscious mtaani watu buuu, ongea ongea tu mafumbo uoga, sikio halipimi neno kama ulimi uonjavyo mboga, kama kiporo hakiitaji moto mwingi basi sihitaji nguvu kupambana na hawa ‘wabishi’, anarap Bonta.
Bonta ameendelea na kuwapa dongo Ali Kiba na Ommy Dimpoz akichana: Ukisikiliza Dushelele mimi ntarewind Propaganda na ukipozi Nai Nai mimi ntafanya Manuva kwenye posa kama Langa.”
Usikilize hapa.