Burudani
Bosi wa Kaburu Entertainment afariki dunia
Mkurugenzi wa label ya Kaburu Entertainment, Mr Kaburu amefariki baada kuugua kwa kipindi kifupi.
Taarifa kutoka kwenye familia yake ambazo zimetolewa na mdogo wa marehemu, Tula Mapenzi zimeeleza kuwa Kaburu amefariki jana mchana Moshi ambapo alienda kwa ajili ya kupatiwa matibabu.
“Baada ya kujisikia vibaya akawa ameenda nyumbani Moshi, baaada ya kufika kule akawa amezidiwa akawa amepelekwa hospitali ndio jana mchana akawa amefariki,” imeeleza taarifa hiyo.
Enzi za uhai wake Kaburu aliweza kufanya kazi na wasanii mbali mbaili akiwemo Rich Mavoko, Amber Lulu na wengineo.