Mchezaji wa Klabu ya Simba, Clatous Chama kwa mara ya kwanza amefunguka baada ya timu yake kufungwa goli 5-1 dhidi ya Yanga na yeye kuhusishwa kuwekwa Kikaangano na Mabosi zake kwa tuhuma za uhujuma.
“Katika hali hizi hakuna haja ya kunyoosheana vidole na kuhamisha majukumu haitatusaidia kwa vyovyote vile. Huu ni wakati mwafaka wa kushikana mikono pamoja kuweka mioyo yetu na vichwa pamoja. Twende tena leo kwa roho moja na tufanye kazi ya kujikomboa.”- Clatous Chama
Simba itashuka uwanjani kumkabili Namungo mchezo wa Ligi Kuu kwenye Uwanja wa Uhuru saa 10:00 alasiri