Habari

China: Kujiunga chuo, kujifunza udereva, ukitaka kuoa au kuolewa sharti uchangie damu

Ajali za barabarani duniani hutokea kila uchao, na wahitaji wa damu wanazidi kuongezeka huku idadi ya wachangia damu nayo ikizidi kushuka siku hadi siku na kuleta hatari kwa maisha ya wahitaji.

Chinese-couple

Kutokana na hali hiyo mji wa Baoji nchini China uko kwenye harakati za uhamasishaji uchangiaji wa damu kwa mtindo wa kipekee , kampeni ambayo imewekwa ni kwamba kama unahitaji kujiunga na chuo,ukitaka kujifunza udereva na hata ukitaka kuoa ama kuolewa sharti uchangie damu, kampeni ambayo imezua mjadala mkubwa kwenye mitandao ya kijamii.

Sharia hiyo mpya iliyotambulishwa katika jimbo la Shaanxi mjini,itaanza kutumika rasmi wiki ijayo inawataka askari na wanachuo wa mwaka wa kwanza kuchangia damu walau mara moja kwa mwaka .Wananchi wa China wanaotaka kuomba leseni za udereva,wanaopokea vyeti vya uhitimu wa mafunzo,wanaoajiriwa kwa mara ya kwanza, na wale wanaofunga ndoa kwa msajili wa ofizi za mji wa Baoji wanapaswa kuchangia damu kwa lazima kama mchango wao kwa jamii.

Taarifa hii ilichapishwa katika mtandao na website ya mji huo wa Baoji, lakini kampeni hii imekumbwa na changamoto ikiwemo wakaazi wa mji huo kuhoji damu hiyo inayotakwa kwa mtindo huo wanahoji uchangiaji ukoje na damu hiyo itatumika wapi, badala ya kuifikiria Zaidi sharia hiyo mpya.

Katika jimbo la Pujiang liloko Zheijang wao wameichukulia tofauti kampeni hiyo na hivyo wanaongeza alama za ziada kwa wanafunzi wa sekondari ambao wazazi na walezi wenye utamaduni wa kuchangia damu.

Source:BBC

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents