Habari

Chuo kikuu cha Nairobi chafungwa

Nairobi, Kenya. Chuo Kikuu cha Nairobi kimefungwa kwa muda usiojulikana.

Wanafunzi chuoni hapo waliamriwa ifikapo saa tatu asubuhi leo Jumanne wawe wameondoka chuoni hapo.

Uamuzi huo umefikiwa na Seneti ya chuo kutokana na suala la kiusalama.

Mkurugenzi wa Mawasiliano na Umma wa chuo hicho, John Orindi amesema, “Tutatangaza ni lini chuo kitafunguliwa.”

Uamuzi huo umechukuliwa kutokana na maandamano yaliyofanyika wiki iliyopita ambayo yalisababisha wanafunzi 27 kujeruhiwa.

Chanzo: Mwananchi

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents