Davis Hilary ashinda Tusker Project Fame
Davis Hillary Ntare Kutoka Uganda ndiye aliyeibuka mshindi katika shindao la Tusker Project Fame usiku wa jana katika fainali za mashindano hayo. Peter Msechu, mshiriki kutoka Tanzania alijinyakulia nafasi ya pili katika shindano hilo lilihohusisha nchi za Afrika Mashariki.
Davis amepewa shilling milioni 5 za Kenya, takriban million 90 za kitanzania na vilevile kupata mkataba wa kurekodi na Gallo Records ya nchini Afrika Kusini. Pia amepata mkataba na Premier Health cover country of Resolution Health inayolipia gharama za kiafya na Study bursary kutoka Mranatha.
Fainali za shindano la Project Fame lililofanyika nchini Kenya jijini Nairobi, ambapo Davis Hillary alitangazwa mshindi na Peter Msechu wa pili pia iliona Steve na Amileena kufika katika fainali.