Burudani

Dayna Nyange atoa sababu ya kutoshirikisha wanawake wenzake kwenye nyimbo zake

Wasanii wengi wa kike kwenye muziki hapa Bongo wamekuwa wagumu katika kushirikishana kwenye nyimbo zao, mmoja kati ya wasanii hao ni Dayna Nyange.

Dyna-Nyange

Akiongea na Bongo5, Dayna amesema kuwa kwa sasa ideas nyingi anazokuwa nazo zinahitaji sana wasanii wa kiume pekee.

“Siwezi kusema kuwa nawatenga wasanii wenzangu wa kike kufanya nao kazi, kila kitu kina wakati wake. Nitafanya nao kazi pale nitakapoona inahitajika nifanye nao kazi. Nashindwa kufanya nao kwa sasa kwa sababu idea nyingi ninazokuwa nazo zinahitaji wasanii wa kiume pekee,” amesema Dayna.

“Lakini nashukuru angalau nilishawahi kufanya kazi na Misoji Nkwabi aliyekuwa mshindi wa BSS,” ameongeza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents