Habari

Deni la Marekani kutawala Mkutano wa G7

Mawaziri wa fedha na magavana wa benki kuu kutoka kwenye mataifa saba tajiri ( G7 ) wameanza mkutano wao unaofanyika nchini Japan ambapo wanajadili kuhusu masuala muhimu ya Dunia.

Wasiwasi juu ya kiwango cha juu cha deni la taifa la Marekani umetawala mkutano kutokana na kwamba iwapo nchi hiyo itashindwa kulipa deni lake basi dunia itakumbwa na mtikisiko mkubwa wa kiuchumi.

Waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen amesisitiza kwamba mojawapo ya vipaumbele vyake ni kutatua mgogoro wa deni unaolikumba nchi yake ambapo amelitaka bunge la Marekani kuongeza kikomo cha deni la taifa la dola trilioni 31.4 ili kuepusha hali ya kushindwa kulipa deni ambayo ikitokea itasababisha kuzorota kwa uchumi wa dunia nzima.

Mawaziri hao wa fedha na magavana wa benki kuu kwenye mkutano huo wa G-7, mbali na kuzungumzia juu ya kuiunga mkono Ukraine pia kwenye ajenda yao wanaangazia wasiwasi wa kutokuwepo na uhakika katika shughuli za mabenki pamoja na kusambaratika baadhi ya Benki nchini Marekani na vilevile hofu ya taifa hilo kubwa kushindwa kulipa deni lake la taifa.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents