Burudani
Diva atease ngoma yake ijayo ‘Jicho la Huba’ aliyomshirikisha Stereo na Prezzo
Ulishamsikia kwenye ‘Piga Simu’ na kwenye ‘Mgonjwa kwa Raha Zako’ na sasa jiandae kumsikia tena kwenye ‘Jicho la Huba’.
Kwa mara nyingine tena mtangazaji wa Clouds FM, Loveness Diva aka The Bawse, ameingia tena studio na producer Lamar kutengeneza ngoma hiyo aliyoshirikishwa rapper Stereo.
Diva amefunguka pia kuwa Prezzo atashirikishwa kwenye wimbo huo.
Kwa kionjo hicho kidogo alichotoa, Jicho la Huba ni ngoma kali lakini usipokuwa makini sauti ya Diva humu unaweza kuifananisha kidogo na sauti ya Saraha.