Habari
Dj Aaron aeleza ujio wa ‘All-stars Students Awards
Dj wa zamani wa Clouds FM, Aaron, ameanzisha kile alichokiita All-stars Students Awards.
DJ Aaron akiongea kwenye kipindi cha Morning Trumpet cha Azam TV
Hizo ni tuzo zitakazotolewa kwa wanafunzi wa shule za Afrika Mashariki.
Alhamis hii Dj Aaron alialikwa kwenye kipindi cha Morning Trumpet cha Azam TV kuongelea tuzo hizo zitakazofanyika jijini Dar es Salaam.
Aaron amesema tuzo hizo zina dhumuni la kuwapa hamasa wanafunzi wa shule za Afrika Mashariki. Tuzo hizo zitatolewa kwa wanafunzi watakaofanya vizuri kwenye mitihani ya kidato cha nne na sita.
Masomo yakayotolewa tuzo ni Kiswahili, Hesabu, Fizikia, Kemia, Bailojia na Kiingereza. Mchakato wa tuzo utaanza katikati ya mwezi wa sita.