Official DJ wa @harmonize_tz @djsevenworldwide ametajwa kwenye tuzo kubwa barani Afrika za AFRIMA kupitia wimbo alioshirikishwa na msanii kutoka nchini Uganada @spice_diana.
Mbali ya kuwa DJ lakini pia Seven ameingia rasmi kwenye kiwanda cha muziki wa Bongo Fleva na tayari ametoa ngoma kadhaa akishirikiana na wasanii mbalimbali akiwemo boss wake Harmonize.
Katika kipengele hicho Spice Diana ametajwa kwenye ngoma ya TUJUANE akishindana na wasanii kadhaa wakiwemo Tanasha Dona kutoka Kenya, Nandy kutoka Tanzania na wengine wengi.