Michezo
Djbrill Cisse ametangaza maamuzi haya katika soka
Mchezaji wa zamani wa vilabu vya Sunderland, QPR na Liverpool Djbrill Cisse ambaye saivi ana umri wa miaka 35, ametangaza rasmi kustaafu soka na sasa anaelekeza nguvu na akili katika kazi yake mpya ya uDJ na brand yake ya nguo inayoitwa “Mr Lenoir”.
Djbrill Cisse akiwa katika kazi yake mpya ya DJ
Mfaransa huyo ambaye amekuwa katika soka kwa muda wa miaka 17, amewahi kuvitumikia vilabu 11.
Cisse wakati akiwa na klabu ya Liverpool aliwahi kuchukua kombe la Klabu Bingwa Ulaya (2004-2005).