Burudani

Dogo Janja asema kiama cha playback kimefika

Msanii wa muziki kutoka Tip Top Connection, Dogo Janja amesema kiama cha blayback kimefika hivyo wasanii wajifunze kupiga muziki wa live kwenye show zao.
dogo-janja

Rapa huyo ambaye alifanya show ya live katika tamasha la Fiesta lililofanyika weekend iliyopita, amesema amegundua kuna kitu cha ziada wanapata mashabiki wake kutokana kuimba live kwenye show.

“Kusema kweli nimepata pongezi kutoka kwa watu wengi sana tena wengine sina ushikaji nao,” alisema Dogo Janja. “Kwahiyo kwangu mimi naona kwa sasa ndo muziki unaenda huko, kiama cha playback kimefika, wasanii tubadilike twende kwenye muziki ambao unaweza kupendwa na dunia,”

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Kidebe, amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa mkao wa kula kwaajili ya ujio wa kazi zake mpya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents