Fahamu

Dubai yazindua jengo lingine refu zaidi duniani

Dubai inakuwa ni sehemu pekee duniani ambayo ina majengo marefu zaidi duniani na hii ni baada ya jana Jumapili Februari 11, 2018 kuzindua jengo la Gevora Hotel towers.

Gevora Hotel towers

Jengo hilo lenye ghorofa 75 na urefu wa mita 356 kwenda juu linakuwa ndiyo jengo la Hoteli refu zaidi duniani.

Picha inayohusiana
Gevora Hotel towers.

Hata hivyo, rekodi ya jengo refu la hoteli duniani ilikuwa inashikiliwa na Dubai yenyewe ambapo jengo la hoteli la JW Mariott Marquis ambalo limezidiwa mita moja tu na jengo jipya la Genova Hotel ndio lilikuwa linashikilia rekodi hiyo.

Jengo la JW Mariott Marquis kulia na Gevora Hotel towers kushoto

Jengo hilo la Hoteli ya Genova ina vyumba 528 na kuna klabu kubwa 5 na swimming pool  na migahawa mikubwa 30.

Tokeo la picha la Gevora Hotel towers

Dubai ndiyo sehemu mpaka sasa inayoongoza kuwa na jengo refu zaidi duniani la Burj Khalifa lenye urefu wa mita 828.

 Dubai is also home to the world's tallest building, the Burj Khalifa, which pierces the city skyline at 828 metres (half a mile) high
Burj Khalifa

Kwa mujibu wa mtandao wa  Emirates 24/7 hoteli hiyo litaanza kupokea wageni kuanzia jumatatu ya wiki lijalo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents