HabariMichezo

FIFA yazindua rasmi Uwanja wa michezo wa Pele mjini Kigali

Uliokuwa ukiitwa Uwanja wa michezo wa Nyamirambo mjini Kigali sasa umepewa jina jipyala Kigali Pele Stadium baada ya uwanja huo kufunguliwa rasmi na Rais wa shirikisho la soka duniani (FIFA) Gianni Infantino pamoja na Rais wa Rwanda Paul Kagame.

Uwanja huu umefunguliwa kongamano la FIFA la 73 linalowajumuisha wajumbe 2,000, likitarajiwa kuanza rasmi hii leo mjini Kigali leo.

Ni katika kongamano hili ambapo uchaguzi wa FIFA utafanyika. Rais wa sasa wa FIFA Infantino ndiyo mgombea pekee wa kiti hicho baada ya kutokuwa na mpinzani.

Baada ya uzinduzi wa Uwanja wa Pele wa Kigali washiriki wa Kongamano hilo walicheza mechi ya soka, timu moja ikiongozwa na Rais wa Rwanda Paul kagame huku timu nyingine ikiongozwa na Rais wa FIFAGianni Infantino.

Rais Kagame ambaye anafahamika kama shabiki wa mpira wa migu hususan wa timu ya Uingereza ya Arsenal – ambaye hucheza mchezo wa tenesi, aliwashangaza wengi alipojitokeza uwanjani kucheza soka.

Upande wa timu ya Kagame alikuwemo Jay Jay Okocha wa Nigeria, Patrice Motsepe mkuu wa CAF, Jimmy Mulisa, Kalekezi Olivier, Kayiranga Baptiste, Eric Nshimiyimana bakanyijijeho wa Rwanda ubu bambaye kwa sasa ni kocha, Grace Nyinawumuntu kocha wa timu ya wanawake ya Rwanda, rais wa Shirikisho la soka la Rwanda FERWAFA Olivier Nizeyimana.

Upande wa timu ya Infantino ilikuw ana wachezaji kama Youri Djorkaeff aliyewahi kuchezea timu za Paris Saint Germain na Monaco uambaye kwa sasa ni mshauri mkuu wa FIFA na Gilberto Silva aliyekuwa mchezaji maarufu wa Arsenal.

Timu ya  Kagame iliifunga timu ya Gianni Infantino 3-2, katika mchezo uliosimamiwa na mwamuzi wa kimataifa Salma Mukansanga.

Mwezi January, wakati wa mazishi ya Pele,Infantino, ambaye anamuelezea Pele kama“mwanamichezo wa mfano wa kuigwa”, alliahidi kuiomba kila nchi duniani kuupatia jina la Pelé uwanja, kwa heshima ya Mchezaji bora wa Brazil na dunia. Rwanda, ambayo inapokea kongamano la 73 la FIFA ni miongoni mwa nchi ambazo zimetekeleza ombi hilo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents