Michezo
Gari la mashabiki Yanga lapata ajali, Uongozi Young Africans watoa pole (+Video)
Uongozi wa Yanga watoa pole kwa Wanachama na mashabiki kutoka tawi la Kidali Asilia Tandale waliopata ajali wakiwa njiani kuelekea Morogoro
Uongozi wa Klabu ya Yanga unatoa pole kwa Wanachama na Mashabiki wetu, kutoka tawi la Kidali Asilia Tandale waliopata ajali wakiwa njiani kuelekea Morogoro ambako timu yetu inacheza na Mtibwa Sugar.
Ajali hiyo imetokea eneo la Kingorwila nje kidogo ya mji wa Morogoro imesababisha majeruhi kadhaa na uhalibifu wa mali , hivyo Uongozi unawaombea majeruhi wote wapone haraka.
Uongozi unathamini mchango mkubwa wa Wanachama na Mashabiki katika kuisapoti timu yetu popote inapocheza hapa nchini.
https://www.instagram.com/p/CC8ti0-hTAj/