Burudani

Idris Sultan akanusha kuwahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu

Mshindi wa BBA 2014, Idris Sultan amekanusha kuwahi kutoka kimapenzi na Wema Sepetu baada ya kuonekana kuwa karibu zaidi katika miezi kadhaa iliyopita.

wema na idriss insta

Akizungumza jana kwenye kipindi cha Mkasi TV kinachorushwa kupitia kituo cha runinga cha EATV, Idris alisema hajawahi kutoka kimapenzi na Miss Tanzania huyo wa mwaka 2006 kama watu wanavyosema.

“Kwahiyo mimi nikiwa natembea na Wema haimaanishi kuna kitu chochote kinaendelea, rumors has nothing,” alisema Idris.

Pia Idris alieleza anawezaje kuwa karibu na Ommy Dimpoz, Diamond pamoja na Wema Sepetu wakati wasanii hao hawaelewani. “Kiukweli ni ngumu lakini hawa ni watu ambao mimi nawahitaji kwenye maisha yangu bila kujali sijui kama wao wananihitaji, ni watu ambao walininspire,” alisisitiza.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents