Burudani
Idris Sultan: Mimi na Samantha tumeachana
Idris Sultan na Samantha wa Afrika Kusini hawapo tena pamoja – kwa mujibu wa mshindi huyo wa Big Brother Africa 2014.
Akiongea Jumapili, November 15 kwenye kipindi cha The Playlist cha Times FM, Idris alithibitisha kuwa uhusiano wao umeshavunjika.
Samantha na Idris walikuwa wamefika mbali zaidi kwenye uhusiano wao kiasi cha mrembo huyo waliyefahamiana kwenye shindano hilo kuja Tanzania na kuishi na Idris kwa wiki kadhaa.
Idris akiwa na mtangazaji wa kipindi cha The Playlist, Lil Ommy
“It’s over,” Idris alimjibu mtangazaji wa kipindi hicho Lil Ommy aliyemuuliza kama kuna ukweli wowote kuhusiana na tetesi kuwa amemchumbia.
“Me and her is done,” aliongeza.