Burudani
Izzo Bizness ni baba mpya mjini, tazama picha ya binti yake hapa!!
List ya wasanii/wanahip hop Tanzania waliobahatika kupata watoto inazidi kuongeza sasa. Na sasa chama cha wazazi vijana kinamkaribisha rasmi, Emmanuel Simwinga aka Izzo Bizness kundini.
Mtoto wa kike wa Izzo B
Hitmaker huyo wa Love Me, ameshare picha hiyo ya mwanae kwenye Instagram ambaye anaonekana kufanana naye hasa macho, na kuandika ‘Miss Bizness’.
Bongo5 imethibitisha kwa Izzo B kuwa huyo ni binti yake na amesema ‘hakuna utajiri mkubwa duniani kama wa mtoto’.
Hongera sana Izzo.