Michezo

Jose Mourinho: Katoa maoni yake kuhusu Lionel Messi

Kocha Jose Mourinho hivi karibuni amefanya mahojiano na kituo cha BT Sport na kutoa maoni yake juu ya tofauti ya kuwa na Lionel Messi katika kikosi na kucheza dhidi yake, hasa katika Champions League.

hi-res-dd31f023f37734db8e85eac21a392097_crop_exact

“Messi ameshinda Champions League na makocha tofauti. Nadhani ni rahisi kushinda ukiwa nae kuliko ukicheza dhidi yake,” alisema.

Kocha huyo Mreno bado anaamini kwamba kucheza kitimu – teamwork ni muhimu.

“Mimi ni kocha wa timu ya soka. Najua kwamba wakati mwingine watu wanadhani kwamba mchezaji mmoja mmoja ni muhimu kuliko timu. Bado nafikiri kwamba timu ni muhimu zaidi kuliko chochote. Lakini ni ukweli dhahiri kwamba kuna baadhi ya wachezaji ambao wanaweza kufanya tofauti,” alisema.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents