Burudani

Juma Nature ana wasiwasi wasanii wakongwe watapotea kutokana na kunyimwa nafasi

Juma Nature ana wasiwasi kuwa itafika wakati wasanii kama yeye watapotea kutokana na kutopewa nafasi katika mambo mbalimbali.

Juma Nature

Nature ameiambia Bongo5 kuwa wadau wa muziki na vikundi vya watu vimekuwa vikiwatumia wasanii wa aina moja kila siku na hivyo wasanii wengi akiwemo yeye kutoonekana kabisa.

“Muziki unakuwa lakini kuna wasanii wanabaki pala pale,” amesema Nature. “Wachache ndo wanapata mashavu. Hebu muangilie kama Rich Mavoko ana tatizo gani? Watu wanawatumia wasanii wa aina moja na ndo hao wamekuwa wakiwasapoti na kuwaacha wasanii wengine wakiwa hawana issue. Sasa wewe unategema nini? Kila siku Diamond, Diamond, Diamond kwanini isiwe na Ali KibA au wasanii wote wapewe fursa sawa ili tufike mbali? Mimi sitaki kumlaumu mtu ninachotaka kusema ni kila msanii apewe nafasi,” amesisitiza rapper huyo.

“Unajua wakati sisi tupo Bongo Record, wasanii wote tulikuwa wamoja/ Show tunafanya kwa pamoja na tunagawana kile kinachopatikana kila mtu anaridhika. Sasa hivi muziki umebadilika kabisa, wachache wananufaika na wengine wanaendelea kupotea. Wewe ujiulize wasanii wakongwe wote wapo wapi? Wanapotea.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents