Burudani
Kajala anakuja na filamu ya “Heart Attack”
Mwigizaji wa filamu Tanzania Kajala Masanja ameanza kushoot filamu yake ya kwanza iitwayo ‘Heart Attack’ tangu atoke kutoka mahabusu kutokana na tuhuma zilizokuwa zikiwakabili yeye na mume wake.
Kwa sasa Kajala amenyoa nywele zake zote ikiwa ni moja ya maandalizi ya kushoot moja ya scene ya filamu hiyo ambayo itakuwa ikielezea maumivu aliyokutana nayo katika maisha yake aliyoyapitia. Katika filamu hiyo itawashirikisha Hemedy na mastaa wengine.
Kajala akiwa amenyoa kipara tayari kwa kushoot filamu ya Heart Attack
Akiongea na mtandao wa Bongo Movies Kajala alisema, “nipo nashoot movie yangu mpya ndo maana imenibidi ninyoe kipara maana inanilazimu kuonekana hivyo ndani na filamu hiyo.”