Burudani

Kama dongo hili la Diamond linaenda kwa Mobetto basi hali si shwari!

Rais wa WCB, Naseeb Abdul aka Diamond Platnumz ametema cheche za mwaka mtandaoni huku moja kwa moja wadau wa mambo wakilihusisha tukio hilo na kitendo cha mwanamitindo, Hamisa Mobetto ambaye amejifungua mtoto wa kiume Agosti 8 mwaka huu na kumpachika jina la Abdul Naseeb.

Diamond alimtumia Mobetto katika video ya wimbo wake, Salome uliotoka mwezi Disemba mwaka jana.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Eneka, ameonyesha kuchukizwa na baadhi ya mambo yanayoendelea.

“BITCH IS DYING FOR FAME,” alitweet Diamond.

Wadau wa mambo wanadai kauli hiyo imekuja baada ya Mobetto kumpatia mtoto wake jina Abdul Naseeb hali ambayo imewafanya watu wengi watambue kwamba mtoto huyo aliyejifungua hivi karibuni ni wa Diamond ambaye kwa sasa ni baba wa watoto wawili aliyozaa na Zari The Bosslady.

Diamond hajawahi kutoa kauli yoyote kuhusiana na tukio hilo licha ya mama yake pamoja na dada yake Asma kuonekana mara kadhaa katika hospitali aliyojifungua mwanamitindo huyo.

Mashabiki katika mitandao ya kijamii wamekuwa na maoni tofauti juu ya Diamond Platnumz huku wengi wakimshauri muimbaji huyo kumkubali mtoto kwa madai Mobetto ni mtu mzima na anatambua kile anachokifanya.

Kwa upande wa Mobetto huyo ni mtoto wake wa pili ambapo wa kwanza alizaa na Mkurugenzi wa EFM, Majay.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents