Habari

Kenya: Madereva walevi kupewa adhabu ya kufanya kazi mochwari

Mamlaka ya Usalama wa Uchukuzi nchini Kenya NTSA imependekeza adhabu mpya miongoni mwa madereva walevi.

Madereva walevi sasa watalazimika kufanya kazi katika vyumba vya kuhifadhia maiti ili kupunguza idadi kuu ya ajali za barabarani.

”Hatuwezi kuwa na madereva wengi walevi wanaofanya ajali na wanapofikishwa mahakamani wanapewa adhabu hafifu.Tutakapokamilisha kutengeza sera hiyo mpya tutahakikisha kuwa inakuwa sheria”, alisema mkurugenzi wa mamlaka hiyo Francis Meja.

Na Wakenya wengi katika mitandao ya kijamii waliunga mkono mpango huo na kusema kuwa utawafanya madereva kuwa makini.

Je una hisi sheria hii ikija Tanzania itasaidia kupambana na madereva walevi?.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents