Michezo
Koeman: Siwezi kushangaa kwa sababu hii ni mara ya tatu mfululizo napata ushindi dhidi ya Wenger
Kocha wa klabu ya Everton Ronald Koeman amemshangaa kocha Arsene Wenger kwa kulalamikia uamuzi wa refa Mark Clattenburg, baada ya Everton kupata ushindi dhidi ya Arsenal kwa mabao 2-1.
Wenger alihisi kua kuna namna ambayo ilichangia ushindi wa Everton haikuwa sahihi.
Siwezi kushangaa kwa sababu hii ni mara ya tatu mfululizo nimeshinda dhidi ya Arsenal na mara ya tatu mfululizo refa amelaumiwa alisema Koeman.
Ushindi mara mbili Koeman alipata dhidi ya Arsenal, aliupata wakati akiongozo klabu ya Southampton ambayo ilishinda kwa mabao 4-0 mwezi Desemba mwaka 2015 na kwa mabao 2-0 miezi 11 baadaye.
Kocha Wenger ameshindwa kumshinda Koeman katika mechi nne zilizopita.