Michezo
Kyle Edmund atupwa nje ya michuano ya Chengdu Open
Michuano ya wazi ya Tenis nchini China ya Chengdu imeendelea tena ambapo muingereza, Kyle Edmund ameshindwa kutamba mbele ya Jared Donaldson baada ya kukubali kipigo kikali katika mchezo wa duru la pili.
Edmund ambaye alifanikiwa kumtoa, Bernard Tomic katika mchezo uliyopita amekubali kipigo cha jumla ya seti 6-0, 1-6, 6-4 kutoka kwa Jared Donaldson raia wa Marekani.
Kyle Edmund arejea kwa kishindo michuano ya Chengdu Open
Mashindano hayo ya wazi ya Chengdu ‘Chengdu Open’ inaendelea tena leo siku ya Alhamisi kwa michezo kadhaa kupigwa wakati mchezaji, Taylor Fritz atashuka dimbani kukipiga na Nikoloz Basilashvili, Dominic Thiem dhidi ya Guido Pella.