Michezo
Ligi ya Europa: Timu ya Samatta yapangiwa na kigogo wa Hispania
Hatimaye, Ijumaa hii shirikisho la soka Ulaya (Uefa) limezipanga timu 48 katika makundi 12 zitakazochuana kwenye michuano ya ligi ya Europa.
Michuano hiyo inatarajiwa kuanza Septemba 15 mwaka huu, huku timu ya Mbwana Samatta, KRC Genk ikipangwa kundi F pamoja na timu za Athletic Bilbao, Rapid Wien na Sassuolo.
Wakati huo huo mchezaji wa Fenerbahce ya Uturuki, Robien Van Persie anatarajiwa kukutana na timu yake ya zamani ya Manchester United zilizopangwa kundi moja kwenye michuano hiyo.