Habari

Maandamano ya kumpinga Donald Trump yaingia siku ya pili

Maelfu ya watu wanaopinga ushindi wa Donald Trump kwenye uchaguzi wa Urais, wameendelea kuandamana mtaani kwa usiku wa pili sasa katika miji mbalimbali nchini Marekani.

3a3925f600000578-3923346-people_march_and_shout_during_an_anti_trump_protest_in_oakland_c-a-18_1478798612240

Waandamanaji wa huko Portland, Oregon, walikabiliana vikali na polisi. Kile kilichoanza kama maandamano ya amani ya watu zaidi ya 4,000, kimegeuka kuwa na fujo.

3a38993c00000578-3923346-a_protester_shoots_fireworks_at_police_officers_during_rioting_i-a-20_1478798612413

Watu hao wameharibu biashara, magari na kuwatupia vitu polisi. Maandamano mengine yanaendelea kwenye miji ya Los Angeles, Philadelphia, Denver, Minneapolis, Baltimore, Dallas na Oakland, California.

Rais huyo mteule, Trump ameyalaani maadamano hayo.

“Just had a very open and successful presidential election. Now professional protesters, incited by the media, are protesting. Very unfair,” aliandika kwenye Twitter.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents