HabariSiasa

Mali, Burkina Faso zaondolewa vikwazo na ECOWAS

Viongozi wa Afrika Magharibi waliokuwa wakihudhuria mkutano wa kilele wa kanda hiyo wameamua kuziondolea vikwazo vyote vya kifedha na kiuchumi Mali na Burkina Faso.

Haya yamesemwa na Jean Claude Kassi Brou, mwanasiasa wa Ivory Coast ambaye amekuwa akihudumu kama rais wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi ECOWAS.

Brou lakini amesema nchi hizo mbili bado zimefungiwa uanachama wake wa ECOWAS. Rais huyo amesema Guinea bado haijaondolewa vikwazo vyovyote vile kwa kuwa haikuwasilisha mkakati uliokubalika utakaoipelekea nchi hiyo kufanya uchaguzi utakaorudisha utawala wa kiraia.

Brou ameeleza kuwa nchi zote tatu zitarudi kuwa wanachama wa Jumuiya hiyo ya Afrika Magharibi mara tu zitakapofanya uchaguzi.

Kuathirika vibaya kwa uchumi kutokana na vikwazo vya fedha

Jeshi la Mali limeahidi kufanya uchaguzi mnamo Machi 2024 pendekezo lililokubaliwa ingawa mjumbe mmoja wa ECOWAS amesema hakuna mwanajeshi yeyote atakayekubaliwa kugombea urais katika uchaguzi wowote ujao nchini Mali.

Mali iliwekewa vikwazo vya kibiashara na kifedha mnamo mwezi Januari, jambo lililopelekea nchi hiyo maskini ambayo haina bahari na ambayo uchumi wake ni duni tayari kutokana na mapigano ya kijihadi yaliyodumu kwa miongo kadhaa.

Nalo jeshi la Burkina Faso limeomba kipindi cha mpito cha miaka miwili kabla kufanya uchaguzi. Jeshi hilo vile vile limesema litafanya kura ya maoni ya katiba mwezi Desemba mwaka 2024 na uchaguzi wa bunge na rais Februari 2025.

Akiizuru Ouagadougou kwa mara ya kwanza katika kipindi cha mwezi mmoja, mpatanishi wa ECOWAS Mahamadou Issoufou alimsifu mkuu wa jeshi Luteni Kanali Paul-henri Sandaogo Damiba na serikali yake kwa uwazi wao katika majadiliano.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents