Burudani
Man Fongo: Sipendi mahusiano ya kimapenzi na wanawake mastaa
Muimbaji wa muziki wa Singeli nchini anayefanya vizuri na wimbo wake wa “Hainaga Ushemeji”, Man Fongo ameeleza kuwa hapendi kuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanawake maarufu.
Alisema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha The Base cha ITV.
“Katika ndoto zangu mimi,napenda kuwa na mtu wa kawaida ambaye sio superstar, ndio maana nikaamua kuoa mapema,” alisema Man Fongo alipoulizwa kama kuna msanii yeyote anayetamani kutoka naye kimapenzi.