Burudani
Manispaa ya eThekwini (Durban) kuwalipa Nicki Minaj na T.I. zaidi ya milioni 521 kufanya show
Manispaa ya eThekwini ambamo ndani yake kunapatikana jiji la Durban nchini Afrika Kusini, imedai kuwa inatarajia kutumia R3.7m (zaidi ya shilingi milioni 521) kuwalipa Nicki Minaj na T.I. wanaotarajiwa kutumbuiza mwezi huo.
Maafisa wa manispaa hiyo walieleza taarifa hiyo kwenye mkutano mkuu ambapo fedha hizo zitasaidia kuwaleta wasanii hao jijini Durban.
Rapper huyo wa Live Your Life atatumbuiza Durban March 11. Ziara ya Nicki Minaj itafanyika March 20.