Burudani
Martin Kadinda Kuipeleka ‘Kwachu Kwachu’ kwa mara ya kwanza Arusha
Mbunifu wa mavazi nchini, Martin Kadinda amesema sasa ni zamu ya wakazi wa Arusha kuona mitindo yake ya Kwachu Kwachu.
Martin Kadinda
Kadinda amesema ataonesha mitindo hiyo katika tamasha la Jambo Fashion Festival ambapo itakuwa ni mara ya kwanza kufanya show mkoani Arusha. Martin amesema kuwa kwa sasa bado bado kwachu kwachu inafanya vizuri na watu wameipokea vizuri. Hata hivyo, amedai kuwa baada ya mwaka mmoja ndipo mavazi mapya. “Unajua hivyo ndo huwa nafanya kama ilivyo kuwa kwa Single Button na sasa hii kwachu kwachu,” amesema.
Jambo Fashion Festival litafanyika tarehe 5 October.