Michezo
MASHEMEJI DARBY: Bongo Movie wainyuka Bongo Fleva
Mechi ya ufunguzi wa fainali ya SportPesa Super Cup kati ya wasanii wa Bongo Movie na Bongo Fleva imemalizika muda mchache iliopita hapa Uwanja wa Uhuru kwa wasanii wa Bongo Movie kuondoka na ushindi wa goli 1 bila dhidi ya Bongo Fleva.
Wasanii wa BongoFleva
Goli hilo lililopatikana katika kipindi cha kwanza lilifungwa na Jimmy Mafufu. Hayo yote ni maandalizi ya fainali SportPesa Super Cup iliyozikutanisha timu pinzani za Kenya, AFC Leopard na Gor Mahia ‘Mashemeji Darby’. Angalia picha za mchezo huo.