Burudani

Mimi Mars aungana na Vanessa Mdee, ‘Ila napenda kuwa mama’ (+video)

Baada ya Vanessa Mdee kusema kwa sasa hayupo tayari kuwa na mtoto, Mimi Mars naye pia amefunguka kuhusu hilo.

Mimi Mars amesema kupata mtoto au kuwa mama wa familia ni kitu ambacho wanakihitaji ila ni kwa kipindi cha mbeleni zaidi takribani miaka mitano ijayo.

“Mimi baada ya miaka mitano hivi itakuwa fresh, huku mbele anaweza nikawa mama mwenye familia labda nimeolewa Mungu akijalia lakini napenda sana watoto, napenda sana kuwa na familia na ninapenda kuwa mama familia, so hicho ni kitu kipo kwenye plan zangu,” Mimi Mars ameiambia Bongo5.

Vanessa Mdee na Mimi Mars ni mtu na dada yake na wote wanafanya kazi zao za muziki kupitia label ya Mdee Music pamoja na Brian Simba. Mimi Mars kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Papara’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents