Burudani

Morocco na Tanzania zitashirikiana kimuziki zaidi, asema Meneja wa msanii aliyeshinda tuzo ya Afrima 2016 (Dj Van)

Meneja wa Dj maarufu wa nchini Morocco, DJ Van, amesema ushirikiano ulioanzishwa kati ya nchi yake na Tanzania baada ya mfalme wao Mohammed V kuja nchini hivi karibuni, una nafasi nzuri kwa wasanii wa nchi hizo kushirikiana pia.

b760a28e-12f6-4cd0-9a0c-dbf168647b6b
Nikiwa na Janatte Haddadi (meneja wa DJ Van) na Diamond jijini Lagos

Morocco ndio nchi inayoongoza kwa kuwa na wasanii wakubwa na waliofanikiwa zaidi katika nchi za Kaskazini mwa Afrika. Meneja huyo, Janatte Haddadi, ameiambia Bongo5 kuwa baada ya kusikia taarifa kuwa wananchi wa Morocco wanaweza kuja Tanzania bila visa, walifurahi na kwamba watakuja kwa wingi.

“Sanaa na utamaduni huwaweka watu karibu, hivyo kama tutaweza kufanya kitu na Diamond bila shaka, itafungua connection kati ya Tanzania na Morocco,” alisema Haddadi.

“Itafungua milango kwa watu katika nchi yenu na kwa watu wangu pia,” ameongeza.

01bb44ae-343a-402f-8169-f5b5b278ab62
Janatte Haddadi (kulia) akiwa na wenzake kutoka nchini Morocco kwenye tuzo za Afrima

Haddadi amedai kuwa ni muhimu sasa kukawepo na ukaribu wa kumuziki katika nchi za Afrika Kaskazini na zingine za Kusini, Mashariki na Magharibi.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents