Habari

Mtangazaji wa BBC afariki dunia

Mtangazaji wa kituo cha BBC Radio 5 LiveĀ  na mchezaji mkongwe wa Uingereza, Jimmy Armfield amefariki dunia baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa saratani.


Armfield amefariki akiwa na umri wa miaka 82, alikuwa akifanya kazi ya utangazaji na uchambuzi katika kituo cha BBC Radio 5 Live, nchini Uingereza.

Familia ya mtangazaji huyo mkongwe na mwenye heshima kubwa Uingerez,a imethibitisha kutokea kifo cha mpendwa wao kilichotokea Trinity Hospice mapema asubuhi ya leo.

Enzi za uhai wake aliwahi kuichezea timu ya Blackpool lakini pia alikuwa nahidha wa timu ya taifa ya Uingereza. Na baadae akaenda kuwa kocha wa timu ya Leeds na Bolton, kabla ya kuhamia katika masuala ya utangazaji.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents