Burudani
Nakuja na project itakayowatikisa rappers wengi – Stamina
Stamina amedai kuwa atafunga mwaka kwa wimbo ‘Fundi Mistari’ ambao anaamini utawatikisa rappers wengi.
“Sitoi tena ngoma official kama nilivyosema ila kuna ile albamu itatoka wiki ijayo,” ameiambia Bongo5.
“Pia kuna project mpya nakujanayo ambayo itawateteresha marapa wengi sana. Hii project inaitwa ‘Fundi Mistari’. Kwahiyo ni kama mistari sita ambayo nimechana bila chorus na nitashoot kama kilinge halafu itatoka kwaajili ya watu wanaopenda muziki wangu,” ameongeza.