Habari

Ndege aina ya Boeing 737 iliyosababisha ajali yaruhusiwa kuanza tena safari za abiria

Mkuu wa Mamlaka ya Safari za Anga Marekani (FAA), Steve Dickson, ametia saini agizo linaloruhusu ndege aina ya Boeing 737 kuanza tena safari zake kwa abiria.

Bwana Dickson alisema ana uhakika wa asilimia 100 juu ya usalama wa ndege hizo ambazo zilipigwa marufuku kusafiri baada ya kutokea kwa ajali mbili za abiria nchini Indonesia na Ethiopia, na kusababisha vifo kwa watu 346.

Uamuzi huo wa Mamlaka ya Safari za Anga Marekani (FAA), unamaanisha kuwa ndege hizo zinaweza kuanza tena safari za abiria kufikia mwisho wa mwaka huu.

Mamlaka hiyo imetoa wito marubani kupewa mafunzo zaidi ili waweze kutumia kwa ubora wa juu kifaa kipya cha usalama kilichowekwa kwenye ndege aina ya Boeing 737.

Aidha, wamiliki wa ndege ya Boeing wamefurahishwa na hatua ya FAA na kusema kuwa imejifunza kutokana na makosa yake yaliyotokea awali.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents