Burudani
Ni marufuku wa Dogo Janja kufanya haya kwa wazazi wake
Dogo Janja hawezi kutoboa masikio au kujichora tattoo kama wasanii wengi wanavyofanya – lasivyo hatoweza kukanyaga kwao!
Rapper huyo wa Arusha amesema akithubutu kufanya hivyo atakuwa ameikosea sana familia yake.
“Baba yangu na mama yangu wakati naingia kwenye muziki waliniambia fanya muziki lakini usije ukatoboa masikio, usije ukachora tattoo,” alikiambia kipindi cha Siz Kitaa cha Clouds TV.
“Nikichora tattoo au nikitoboa masikio ni vita nyumbani,” alisema.