Nico Rosberg ashinda mbio za Singapore Grand Prix
Nico Rosberg, dereva wa Mercedes, amefanikiwa kuwa wa kwanza katika kufuzu Singapore Grand Prix, ameshinda mbio hizo ambazo ni mbio zake za 200 katika Formular 1.
Rosberg ambaye hii ni mara yake ya kwanza kushinda Singapore Grand Prix ,huu ni ushindi wake wa 3 mfululizo na wa 8 katika msimu huu wa Formular 1.
Daniel Ricciardo wa Redbull amekamata namba 2 huku bingwa mtetezi Lewis Hamilton ambaye alipata tatizo la breki katika gari lake amekamata nafasi ya 3.
Bingwa wa Singapore Grand Prix mwaka jana Sebastian Vettel wa Ferrari ambaye leo alianza wa mwisho kufuatia kupigwa penati lakini akamaliza mbio akiwa namba 5.
Ushindi wa Rosberg leo umemfanya apae kileleni katika msimamo wa madereva msimu huu akiwa na pointi 273 na Hamilton sasa yupo namba 2 akiwa na pointi 8 nyuma ya Rosberg.