Utani wa Kocha wa Klabu ya Simba SC ambaye pia amewahi kuifundisha Real Madrid, Pablo Franco alivyomtania mwandishi aliyevaa jezi ya Barcelona klabu ambayo ni watani wao wa jadi pale Hispania.
Pablo ameonyesha utani huo wakati wa mechi yao na Red Arrow uwanja wa Mkapa, 21/11/2021 mchezo ambao Simba waliondoka na ushindi wa magoli 3-0.
Mhispania huyo alionekana kutikisa kichwa kama vile anamsikitikia mwandishi huyo huku akitabasamu kwa kukutana na jezi ya watani wao Barcelona ikiwa imevaliwa Tanzania.