Michezo
Cristiano Ronaldo aonesha mapenzi kwa shabiki aliyevamia uwanjani na kumkumbatia
Mchezaji wa klabu ya Real Madrid, Cristiano Ronaldo akiwa kwenye mechi ya ligi ya mabingwa wa Ulaya dhidi ya PSG iliyochezwa jijini Paris, Ufaransa ameonesha mapenzi ya juu kwa shabiki aliyevamia uwanjani.
Shabiki huyo alivamia uwanjani wakati Madrid ikipambana na PSG na alipomfikia Ronaldo, alimpokea na kumkumbatia.
Hata wakati walinzi wa uwanjani wanaingia ili kumtoa, Ronaldo aliwazuia wasimpe kipigo. Badala yake Ronaldo alipiga naye story sekunde kadhaa na kuwaruhusu wamchukue lakini si kwa kumpiga.
Baada ya kitendo hicho mashabiki walimshangilia kwa kile alichoonyesha kwa shabiki huyo aliyeonesha mapenzi makubwa kwake.