Picha: Diamond, Zari the Boss Lady watua Dar pamoja, wapiga selfie za kutosha safarini
Guess nani aliyekuja kwenye ndege moja Dar es Salaam na Diamond… ni mwanamuziki/mfanyabiashara anayedaiwa kuwa mrembo zaidi nchini Uganda, Zari the Boss Lady! Diamond alikuwa anatokea nchini Afrika Kusini alikoenda kushoot video pamoja na Waje. Zari huishi huko na anamiliki chuo.
Diamond na Zari
“Guess who is sitting next to me on this flight to TZ,” ameandika Zari kwenye picha aliyoweka Instagram.
Wawili hao walijikuta wakiwa kwenye siti moja na walionekana kufurahia kampani ya pamoja na kwakuwa wote ni wapenzi wa picha, safari ilikuwa fupi!
“When a flight is boring and there is 2 people who love pics what happens? #SelfieTingz @diamondplatnumz,” ameandika Zari kwenye picha moja wapo kati ya alizoziweka kwenye Instagram.
Baada ya kutua na kupiga picha ya mwisho na kwa kujua kuwa picha hizo zinaweza kuzua tetesi za uhusiano, Zari aliandika: Flight was great…… don’t spread false rumors.