BurudaniPicha

Picha: Vanessa Mdee atumbuiza na 2 Face kwenye show ya Buckwyld N Breathless, Lagos

Katika sehemu ambayo Vanessa Mdee ameshalikita jina lake vyema nje ya Tanzania, basi ni Nigeria.

14052650_265827230482621_1149670948_n

Muimbaji huyo wa ‘Niroge’ Jumamosi hii alikuwa mmoja wa waimbaji walioipamba show kubwa ya msanii mkongwe wa Nigeria, 2 Face Idibia iliyopewa jina, Buckwyld N Breathless. Show hiyo ilifanyika Eko Hotels & Suites, jijini Lagos.

14135101_1751452555138222_1959659388_n

Vee ambaye alitengeneza pair iliyovuma zaidi kwenye Coke Studio Afrika mwaka jana na 2 Face, hakuwa mchoyo wa fadhila kumshukuru muimbaji huyo kwa nafasi aliyompa.

“This picture describes everything I was feeling last night,” ameandika Vanessa kwenye picha akiwa na 2 Face jukwaani aliyoiweka Instagram.

“I thankyou @official2baba for constantly inspiring and elevating youngns like myself. I’m humbled and eternally gratefully.”

14145535_524027424470371_390091245_n

2 Face amewahi kukaririwa akimtaja Vanessa kuwa ni mmoja wa waimbaji anaowakubali Afrika.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents