Habari
Rais wa Ufilipino Rodrigo Durtete atangaza kustaafu siasa 2022
Rais wa Ufilipino, Rodrigo Durtete, ametangaza kustaafu siasa baada ya muda wake wa sasa kumalizika ikiwa ni siku moja tu tangu Mwanamasumbwi Manny Pacquiao kuwasilisha cheti cha kugombea Urais katika uchaguzi uliopangwa kufanyika mwakani.
Durtete amesema kwa sasa anataka kumtengenezea nafasi mtoto wake Sarah ili kuja kuwa kiongozi wa juu.
Awali zilitoka taarifa kwenye baadhi ya vyombo vya habari nchini Ufilipino vikidai kuwa Durtete angeweza kuwa Makamu wa Rais wa Rais atakayeshinda katika uchaguzi wa 2022.