![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2016/08/2014-06-28-17-27-48.jpg)
Rapper King Kapita amefahamika zaidi kwa msaada anaotoa kwa mastaa wa Bongo pindi akaunti zao za Instagram zinapodukuliwa (hacked).
Hafanyi kwa kubahatisha bali hiyo ni fani aliyoisomea Afrika Kusini na Botswana alikojipatia elimu ya IT na kujikita zaidi kwenye security.
Amedai kuwa baada ya kurejea Tanzania alikuta kuna tatizo la hackers na kumlazimu kusoma vyema mifumo ya Instagram na tangu hapo amekuwa akisaidia mastaa kibao.
Anasema kurudisha akaunti zilizochukuliwa huhusisha kuwasiliana na developer wenyewe wa Instagram ambao humsaidia kuzirejesha.