Burudani
RECAP: Cheka tu imefanya Mapinduzi ya Comedy (Video)
Kupitia kwenye kipindi chake cha RECAP & MANDO @el_mando_tz ameizungumzia platform ya CHEKA TU.
Kwanza amewapongeza waanzilishi wa Cheka Tu na kusema kuwa Platform hiyo imekuja kuwa mwokozi kwa maisha ya vijana wengi sana.
Kwa sasa Tanzania Comedy imekuwa moja ya sehemu ya Ajira tofauti na miaka mitatu iliyopita ambapo wengi walikuwa bado hawaiamini.
Lakini pia Cheka Tu wamekuja kuwafanya Watanzania waweke imani kwenye upande wa Uchekeshaji tofauti na zamani.
Kwa sasa Show za Uchekeshaji zinajaza kwenye kumbi kubwa sana na hii yote ni kwa sababu Cheka Tu wamewaaminisha wengi.
Uchambuzi mzima upo katika akaunti yetu ya YouTube ya Bongofive.