Rockstar 4000 yakanusha Ommy Dimpoz kulazwa ICU ‘Ni mzima wa afya na hajalazwa’
Baada ya taarifa kusambaa katika mitandao ya kijamii zikidai kwamba msanii Omary Nyembo maarufu Ommy Dimpoz kuwa amelazwa hospitali katika chumba cha uangalizi maalum (ICU), uongozi wa kampuni inayomsimamia muimbaji huyo imekanusha taarifa hizo.
Akizungumza na MCL Digital leo Jumamosi Agosti 25, 2018, meneja wa msanii huyo Seven Mosha amesema hali ya msanii huyo kwa sasa inaendelea vizuri.
Amesema Ommy Dimpoz alifanyiwa upasuaji wa koo miezi minne iliyopita na tangu hapo hali yake imekuwa ikiendelea vizuri hadi sasa.
“Juzi alikwenda hospitali kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi kwa kuwa kila baada ya miezi mitatu anatakiwa kurudi hospitali ili kuangalia maendeleo yake kama tulivyoelekezwa na madaktari,” amesema Mosha.
Alipoulizwa kuhusu taarifa zinazosambaa kuwa amelazwa ICU, Seven amesema hazina ukweli.
“Dimpoz ni mzima wa afya na hajalazwa, yupo nyumbani baada ya uchunguzi,” amesema na kusisitiza kuwa madaktari kutoka Hospitali ya Milpark iliyopo nchini Afrika Kusini wanamhudumia vyema
Mwanamuziki Madee leo katika ukurasa wake wa Instagram aliweka picha ya Ommy Dimpoz na kuandika, “Kwenye maombi yetu ya kila siku tusimsahau Omary .. tumuombee apone haraka aendelee na majukumu yake ,Omary anaumwa. Tuseme Amen.”
Mtangazaji wa kipindi cha Shilawadu, Soudy Brown naye ameandika, “Omary upo ICU? Haiwezekani huko sio kwako fight, pona mzee baba, pona uje shilawadu tukutoe povu kama zamani, pona urudi gym kama zamani, pona urudi jukwaani kama zamani, pona uje u record mangoma kama zamani.”
Source: Mwananchi
wabongo tumezid kuwazushia wasanii
Wasitufanye watoto sisi kila mtu anamtakia kheri aponee afuu
Mbona sielewi
Nyie si ndo mnaua watu kila siku na kuwafufua kwaupuuzi wenu mkidhani mnafanya vizuri.
Kisa Diamond kamtakia pole msanii mwenzake basi wanakuaja kuleta siasa zao hao rockstar hadi kwenye afya za watu
Binadam wabaya sana sasa na hiz Pole zetu zinaenda wap mwaona raha kutufanya wajinga
Duuuh yaleyale
Rock star ni wehu,omy alikuwa hoi na anaumwa kansa ya koo,na ole wenu afe nyie rock star ,mnacheza na afya ya mtu JINGA KWELI NYINYI
Apone
Ata uyo diamond wenu alikua wapi adi Leo amtakie pole?,kueni na Akili yakuwaza
Ommy dimpoz ana cancer kwenye koo na itabidi wamwondoe shingo nzima wamweke nyingine, ina srmekana hajapata wakujitolea ampe shingo ya spair
Mnatuchanganya…
Faru Jeuri we fara nini siasa gani sasa na ukweli ndio huo mtu kaenda fanyiwa chek up mnamzushia icu waliopost wote wamepost kimihemko tuu wangepost kipindi anafanyiwa upasuaji miezi mitatu nyuma
Mficha maradhi kifo humuumbua
Waandishi wa habari bana,,,
Drim Bway Defya wanazngua hao achana nao
Pray you continue good health Ameen 🙏🙏🙏🙏🙏🙏